AK sasa yasema bajeti ya Olimpiki itatolewa Desemba

109

Rais wa Shirikisho la Riadha nchini Kenya – Athletics Kenya Jackson Tuwei, anadai kuwa bajeti ya kikosi kitakachoiwakilisha Kenya katika michezo ya Olinpiki itatolewa mwezi ujao baada ya kukamilisha majaribio.

 

Kamati ya Olimpiki nchini Nock inatarajiwa kutangaza bajeti rasmi ya timu zote za Olimpiki ili kuwezesha maandalizi kabambe kabla ya michezo hio ya Japan, mwaka ujao. Zaidi ya wachezazi 100 wanatarajiwa kupeperusha bendera ya Kenya katika michezo hio iliyokumbwa na utata mkubwa.

Author: Bruce Amani