Aliyekuwa mkuu wa riadha Kenya apigwa marufuku miaka kumi

78

Kocha wa  wanariadha wa timu  ya  taifa  ya  Kenya  katika michezo ya  Olimpiki ya  mwaka  2016 mjini Rio de Janeiro amepigwa  marufuku kwa  miaka  10 kushiriki  mchezo  huo kwa  kutoa  taarifa  ya  mapema ya uchunguzi  wa matumizi ya dawa  zinazoimarisha  misuli, doping, kwa  wanariadha  ili  kujipatia  fedha. Michael Rotich amepigwa  marufuku , na  kutozwa  faini ya  dola 5,000 leo, na  bodi  ya  maadili  ya  shirika  la  vyama  vya  riadha duniani IAAF baada  ya  uchunguzi  wa  miaka  mitatu.

Rotich alionekana  katika  kamera  akitoa ombi  hilo kwa  mwandishi  habari za uchunguzi kutoka  gazeti la  Sunday Times  la  nchini  Uingereza, ambalo lilitoa  vidio hiyo wakati  wa  michezo  ya  mjini  Rio. Ujumbe  wa  Kenya  katika  michezo  hiyo  ulimrejesha  Rotich nyumbani kutoka  Brazil.

Author: Bruce Amani