Kitendawili cha robo fainali ya Ligi ya Europa kimeteguliwa rasmi. Baada ya hatua ya 16 bora kukamilika na kila timu kuwa gizani katika kutambua mpinzani wake katika hatua ya nane bora.
Droo hiyo imekamilika ambapo Manchester United imepangwa kupepetana vikali na Granada inayoshiriki Ligi Kuu nchini Hispania na mechi nyingine arsenal watacheza na Slavia Prague.
Ajax watacheza dhidi ya Roma na Dinamo Zagreb itachuana na Villarreal.
Katika hatua ya robo fainali, mshindi wa mechi ya Granada na Manchester United atacheza na mshindi baina ya Ajax au Roma na mshindi wa mechi ya Dinamo Zagreb dhidi ya Villarreal atacheza na mshindi wa mechi ya Arsenal au Slavia Prague.
Mechi mbili za robo fainali zitachezwa kuanzia tarehe 8 kwa mkondo wa kwanza na mkondo wa pili itakuwa Aprili 15.
Wakati nusu fainali itakuwa tarehe 29 Aprili na 6 Mei.
Mabingwa watetezi wa michuano ya klabu bingwa Ulaya Bayern Munich watachuana na Paris St-Germain katika…
Droo ya hatua za mwisho za Europa League imefanyika katika makao makuu ya UEFA mjini…
Michuano ya hatua ya robo fainali, kuwania Kombe la klabu bingwa – CAF Champions League…
Rafael Nadal amefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya fainali za ATP kwa kumbwaga mshindi…
Ni mechi ambayo kwa vyovyote vile, walihitaji pointi tatu ili kujihakikishia nafasi ya robo fainali.…
Cameroon imechaguliwa hii leo kuwa mwenyeji wa mechi ya fainali ya klabu bingwa wa soka…