Rais wa La Liga Javier Tebas amesema ana matumaini ya ligi kuu nchini humo kurejea mwezi Juni 12 ambapo anaamini pia kufikia tarehe hiyo hakutakuwa na maambukizi ya virusi vya Corona kwa wachezaji wa vilabu vyote tofauti na ilivyo hivi sasa.
Viongozi wa ligi siku ya Jumapili walitoa taarifa kuwa wachezaji watatu walipimwa na kukutwa wameathirika na Covid-19 katika ligi mbili (daraja la kwanza na pili). Hii inakuja kipindi ambacho wachezaji wa La Liga wameshaanza kurudi katika viwanja vya mazoezi.
“Nitapendelea zaidi kuanza michezo Juni 12,” alisema Tebas.
“Lakini tunatakiwa kuwa makini sana. Ligi inatakiwa ilijee lakini itategemeana na athari za ugonjwa huo katika kipindi hicho kwani hatufanyi hili pekee yetu bali kama jamii ya Kihispania”.
Tebas aliongeza kwa kusema ligi daraja la pili litaanza sawa na ligi kuu kwani mashindano yote nchini humo inatakiwa kumalizika mwishoni mwa mwezi Julai yaani 31 Julai ili kutoa nafasi ya mashindano ya Ulaya kumalizika.
Taifa la Hispania limekuwa miongoni mwa nchi ambazo zimeathirika vibaya na janga la Corona kwani mpaka leo Mei 11 vifo 26,621 na waathirika 264,663 wamesharipotiwa.

Author: Bruce Amani
Related Posts
- Rais wa La Liga nchini Hispania awapinga wanaofuta ligi barani Ulaya
Rais wa ligi kuu ya Hispania La Liga Javier Tebas amesema haelewi kinachoendelea hivi sasa…
- La Liga yatafuta uungwaji mkono wa mchuano wa Miami
Ligi ya Kuu ya kandanda Hispania imeanzisha kampeni ya kuonyesha kuwa mashabiki wa Marekani wanaunga…
- Sevilla yakamata nafasi ya kwanza La Liga
Sevilla imekamata usukani wa La Liga baada ya kupata ushindi wa 1-0 dhidi za Real…
- Bao la Messi lawapa Barcelona taji la 26 la ligi ya Uhispania
Barcelona wamebeba taji lao la 26 la La Liga baada ya kupata ushindi wa 1…
- Mkusanyiko wa patashika ya Ligi ya Premier Jumamosi
Manchester City waliwachabanga Watford mabao 8 - 0 katika mchezo wa Ligi ya Premier. City…
- Droo ya mzunguko wa tatu wa Kombe la Azam yafanyika
Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) Tanzania bara limefikia mzunguko wa tatu, ambapo ni hatua…