Manchester United wamelazimika kutokea nyuma na kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Brighton katika mchezo wa Ligi Kuu nchini England uliopigwa dimba la Old Trafford Leo Jumapili.
Ushindi ambao unaithibitisha klabu hiyo kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao kwa alama ambazo imezikusanya haiwezi kushuka zaidi ya nafasi nne bora.
Brighton walianza kupata goli kupitia kwa Danny Welbeck na kuonekana kama wanaenda kushinda mechi kwa mara ya kwanza katika dimba la Old Trafford.
Hata hivyo, sio mara ya kwanza United kutokea nyuma na kushinda kwa msimu huu, hata leo wamefanya hivyo baada ya kusawazisha bao kwa Marcus Rashford kumalizia pasi ya Bruno Fernandes kabla ya Mason Greenwood kufunga goli akitumia vyema mpira wa Paul Pogba.
Matokeo hayo yanaifanya United kufikisha alama 60 nafasi ya pili kwenye msimamo wa EPL.

Author: Bruce Amani
Related Posts
- Greenwood ajifunga Manchester United mpaka 2025
Mshambuliaji wa kimataifa wa England na klabu ya Manchester United Mason Greenwood ameongeza kandarasi ya…
- Rashford aipa United alama tatu dhidi ya Leicester
Manchester United imepata ushindi wa goli 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya…
- Manchester United wachangamsha mbio za Ulaya kwa kuwabugiza Brighton Hove Albion
Manchester United imepata ushindi wa 15 mfululizo wa ligi baada ya kuichabanga Brighton Hove Albion…
- Manchester United yaambulia ushindi katika mechi ya aina yake dhidi ya Brighton
Katika masaa ya jioni Manchester United imeibuka kidedea dhidi ya Brighton kwenye mchezo wa Ligi…
- Rashford, Martial waingia kambani Manchester United ikishinda 3-2 mbele ya Sheffield
Kikosi cha Manchester United kimefanikiwa kuibuka kidedea wa goli 3-2 dhidi ya kibonde Sheffield United…
- Manchester United yatinga robo fainali Carabao, yatoa dozi kwa Brighton 3-0
Manchester United wamefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya Kombe la Carabao baada ya kuibuka…