Manchester United wanataka kurefusha mkataba wa mkopo wa mshambuliaji wa Kinegeria Odion Ighalo 30, ambaye ametokea Shanghai Shenhua ya China.
Arsenal wana matumaini ya kupata saini ya mlinzi wa Paris Saint – Germain Layvin Kurzawa, 27, baada kuwepo uwezekano mdogo wa kujiunga na miamba ya Catalunya, FC Barcelona.
Liverpool, Southampton na RB Leipzig wako vitani kuwania saini ya winga wa Werder Bremen Milot Rashica, 23, ambaye kandarasi yake inamalizika mwishoni mwa mwezi Juni.
Kiungo mshambuliaji wa Chelsea Tiemoue Bakayoko, ambaye yuko kwa mkopo Monaco anatamani kurudi AC Milan ambako alichezea msimu wa 2018/19 kwa mkopo pia.
Manchester City wanaandaa Euro 32m kwa ajili ya kumsajili mlinzi wa Marseille Boubacar Kamara, 20.
Roma wanaitaka Arsenal walipe nusu ya mshahara (£180000) wa mshambuliaji raia wa Armenia Henrikh Mkhitaryan endapo wanahitaji kweli mchezaji huyo asajiliwe moja kwa moja klabuni Roma.
Hata hivyo The Gunners wapo kwenye mpango wa kumvuta Emirates beki wa RB Leipzig Dayot Upamecano, 21, Tottenham na Manchester United wanavutiwa kumsajili mlinzi huyo pia.
Kufuatia muda wa kuwa kwa mkopo kwa mlinda mlango Loris karius, 26, Besiktas kuvunjwa, mchezaji huyo amepanga kurudi Liverpool ili akamalizie miaka miwili iliyosalia kwenye mikataba.
Huenda kocha Jurgen Klopp angekuwa kocha wa Mexico 2015 baada ya kushawishiwa kwa muda mrefu na taifa hilo kabla ya Klopp kuchukua maamuzi ya kwenda nyumbani kwa Liverpool Anfield.

Author: Bruce Amani
Related Posts
- Manchester United yatinga hatua ya 16 ya Ligi ya Europa
Mshambuliaji mpya wa klabu ya Manchester United Odion Ighalo amefungua rasmi akaunti ya magoli katika…
- Uefa yasema penalti ya United dhidi ya PSG ilikuwa sahihi
Ni penalti iliyogawanya hisia miongoni mwa wengi, lakini sasa Uefa imejitokeza wazi na kuunga mkono…
- City yatinga fainali ya Carabao licha ya kuchapwa na Man United
Mabingwa watetezi wa Kombe la Carabao Manchester City watakutana na Aston Villa kwenye fainali ya…
- Ighalo aipa Nigeria shaba dhidi ya Tunisia
Goli pekee la mshambuliaji Odion Ighalo wa Nigeria limeipa ushindi Super Eagles na kushinda kasi…
- Ighalo aipa Nigeria ushindi mwembamba dhidi ya Burundi
Washindi mara tatu na mabingwa wa mwaka wa 2013 Nigeria walipata ushindi mgumu wa 1…
- Yanga kuivaa Zesco United Ligi ya Mabingwa
Hatua ya pili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika itaendelea wikiendi hii katika…