Tetesi za Mastaa Ulaya: Kocha Pochettino ataka Mbappe kubakia PSG, Man United wamuachia Paul Pogba
Manchester United watamuuza kiungo mshambuliaji wao raia wa Ufaransa Paul Pogba 27 katika dirisha kubwa la usajili la mwezi Juni.
Manchester United hawana uhakika kama dili la kumpata winga wa Borrusia Dortmund Jadon Sancho 20 litafanikiwa mwishoni mwa mwezi Juni baada ya Ole Gunnar Solskjaer kuonyesha matumaini ya kumpata mshambuliaji Erling Braut Haaland.