Alexander-Arnold aliwekwa kando kwenye timu ya taifa ya England na hakuwa sehemu ya kikosi ambacho kilicheza mechi dhidi ya San Marino, Albania na Poland.
Klopp amesema kuwa bado hajaelewa maamuzi ya Kocha wa England, Gareth Sothgate kwa kumuweka kando beki huyo na badala yake kumchukua Kylian Walker wa Manchester City.
Kwa sasa beki huyo amekuwa kwenye wakati mgumu uwanjani ambapo alikuwa kwenye janga la Corona jambo ambalo lilimfanya Klopp asiulize kwa nini aliachwa kwenye kikosi cha timu ya England, Novemba pia alikuwa anasumbuliwa na majeraha lakini kwa sasa anaonekana kuwa yupo fiti.
“Nimeshangazwa namna ambavyo hajawa kwenye kikosi, sikuwa na mpango naye mkubwa katika msimu huu kwa kuwa niliamini kwamba angekuwa kwenye majukumu ya timu ya taifa, ila ajabu ni kwamba hajawa kwenye hicho kikosi jambo ambalo nimeshangaa.
Liverpool inapitia wakati mgumu kwenye mechi nyingi za msimu huu kutokana na wachezaji wake wengi kuwa nje ya viwango pamoja na majeruhi.

Author: Asifiwe Mbembela
Related Posts
- Southgate azawadiwa mkataba mpya
Gareth Southgate amesaini mkataba mpya wa kuendelea kuwa kocha wa timu ya kandanda ya England…
- England yaiduwaza Uhispania
England iliifunga Uhispania 3-2 katika mchuano muhimu wa hatua ya makundi kuwania taji la ligi…
- Kandanda la England kuanza tena kutimua vumbi
Ligi Kuu ya kandanda England, Premier League inarejea wiki hii baada ya kusitishwa kutokana na…
- Klopp awatisha Atletico licha ya kushindwa
Jurgen Klopp amewaonya Atletico Madrid kuwa wasishangilie kuibuka na ushindi wa mchezo wa raundi ya…
- Madaktari England watahadharisha kurejea kwa EPL
Madaktari wa vilabu vinavyoshiriki ligi kuu England wametoa hofu yao ya kurejea kwa ligi baada…
- Beckenbauer anatamani kumuona Klopp akikamata usukani Bayern
Mchezaji nguli wa kandanda wa Ujerumani Franz Beckenbauer amesema kwamba anataka kumuona kocha wa Liverpool …