Mechi mbili za robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ya Chelsea dhidi ya FC Porto itachezwa katika dimba la Seville nchini Hispania kutokana na vizuizi vya Covid-19.
Mitanange hiyo miwili itachezwa katika dimba la Ramon Sanchez-Pizjuan, uwanja ambao hutumiwa na klabu ya Sevilla ambayo inashiriki Ligi Kuu nchini Hispania La Liga.
Mkondo wa kwanza utapigwa Aprili 7 na mkondo wa pili utakuwa Aprili 13.
Awali, mchezo wa raundi ya kwanza wa hatua ya 16 bora wa Chelsea dhidi ya Atletico Madrid ulichezwa Bucharest kutokana na sababu kama hizo.