Timu za taifa za mchezo wa soka kwa upande wa wanawake za Kenya na Tanzania zitamenyana katika fainali ya kuwania taji la nchi za Afrika Mashariki na Kati, CECAFA .
Harambee Starlets iliishinda, Burundi mabao 5-0 katika mechi ya nusu, iliyochezwa leo mchana katika uwanja wa Chamazi jijini Dar es salaam nchini Tanzania.
Miongoni mwa wafungaji ni pampja na Jentrix Shikwanga na Mwanahalima Adam