Timu ya Taifa ya Uganda imetupwa nje ya kuwania nafasi ya kufuzu kuingia Kombe la Mataifa Bingwa Afrika Afcon 2021 Cameroon baada ya kukubali kipigo cha goli 1-0 dhidi ya Malawi mtanange uliopigwa leo Jumatatu Machi 29 Jijini Blantyre.
Matokeo hayo yanalifanya taifa la Malawi kufuzu kuingia Kombe la Mataifa Bingwa Afrika kwa mara ya tatu tangia kuanza kwa mashindano hayo.
Bao pekee katika mechi hiyo limewekwa kimiani na mshambuliaji wa Malawi Richard Mbulu kwa kichwa na sasa wanaifikia rekodi ya mwaka 1984 na 2010.
Malawi wanaungana na timu kutoka Afrika Magharibi ya Burkina Faso kuingia kwenye fainali hizo zitakazofanyika Cameroon mwaka 2022 Januari kutoka Kundi B.
Uganda inaungana na nchi asilia katika umoja wa Afrika Mashariki za Kenya na Tanzania kutofuzu baada ya zote kutinga kwenye fainali zilizopigwa Misri.
Author: Asifiwe Mbembela
Related Posts
-
Maoni: Afrika Mashariki ichukue funzo kufuzu AFCON
Mpira ni hatua. Hatua huwa mithili ya ukuaji wa mtoto kwa maana huwezi kuruka kutoka…
- Uamuzi wa Cameroon kuandaa AFCON waahirishwa
Uamuzi wa kama Cameroon inaweza kuendelea na maandalizi ya kuwa mwenyeji wa kombe la Mataifa…
- Ghana mwenyeji wa AFCON 2018 kwa wanawake
Kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Afrika, CAF imeidhinisha rasmi Ghana kuwa mwenyeji wa…
-
Algeria ndio mabingwa wa Afrika 2019
Goli la dakika ya kwanza ya mchezo la Baghdad Bounedjah limeipa Algeria taji la pili…
-
Staa wa Liverpool Mane alipeleka Senegal AFCON 2022
Staa wa Liverpool Sadio Mane ameipeleka timu yake ya taifa ya Senegal katika fainali za…
-
Stars kibaruani kuikabili Tunisia kufuzu AFCON 2021
Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itakuwa na kibarua cha kumenyana na timu ya…