Amavubi Stars watafuta tiketi ya kucheza Afcon 2022 kwa kuvaana na wenyeji Cameroon

Timu ya taifa ya Rwanda, Amavubi Stars inasaka tikiti ya kufuzu kwenye michuano ya Afcon 2022. Kesho Jumanne ina mtihani  dhidi ya Simba wanyika Cameroon mjini Duala. Ni mchuano unaosubiriwa na wengi  kujua hatma ya Timu ya Rwanda  kama  itafuzu au la.

Kocha mkuu wa Timu ya Rwanda Mashami Vicent  baada ya kuichapa  Msumbiji   bao 1-0 mjini Kigali wiki jana,  aliondoka  ijumaa  na kikosi  cha wachezaji 23 kuelekea Cameroon  kujiandaa kumenyana  na  Simba wa Nyika hapo  kesho  mjini Duala.

Miongoni mwa wachezaji waliorejea ni pamoja na mlinda mlango wao Olivier Kwizera ambaye hakucheza mechi ya Msumbiji kutokana na kadi nyekundu aliyopewa  katika mchuano ya  hatua ya ¼ fainali ya kombe la CHAN 2021 dhidi ya Guinea.

Kocha mashami Vicent ameomba wanyarwanda msaada  wa maombi ili  washinde mechi  hii muhimu dhidi  ya Cameroon.

Katika kundi hili la F, Cameroon wanaongoza  na alama 10, Cape Verde iko kwenye nafasi ya pili na alama 7, Rwanda kwenye nafasi ya 3 na alama 5 wakati Msubiji ikiwa na alama 4.  Endapo  Cape verde watashinda mechi ya ugenini dhidi ya Msumbiji, Rwanda hata ikifunga Cameroon itayaaga mashindano hayo ikifuata Tanzania na Kenya.

Ni michuano inayotarajiwa kuchezwa  mwezi januari na Februari mwakani  nchini Cameroon.

Rwanda ilifuzu kucheza michuano hiyo mwaka 2004 nchini Tunisia. Kama inaweza kurejea  kwa mara ya pili  katika fainali za AFCON 2021 nchini Cameroon.

Author: Bruce Amani