Gueye aipa Senegal tiketi ya robo fainali

Kiungo mkabaji wa Everton Idrissa Gueye ameipeleka timu yake nusu fainali ya mashindano ya Afcon 2019 baada ya kufunga goli moja pekee lililoipa matokeo Senegal kufuzu hatua hiyo katika mchezo uliochezwa Jumatano hii.
Iliwahitaji dakika ya 69 kufunga goli la kwanza baada ya goli kadhaa kukataliwa na wasaidizi wa Marefarii VAR kupitia kwa Mane.
Simba wa Teranga watajilaumu wenye kwa kushindwa kufunga goli mapema kupitia kwa Mane na Niaggh baada ya Benin mda mwingi kuwa nyuma ya mpira.
Hii inakuwa mara ya kwanza kufuzu hatua ya nusu fainali kwa senaggal tangu mwaka 2006. Katika mara tatu iliyoweza kushiriki iliishia hatua ya makundi ambapo.mwaka 2017 iiliishia hatua ua makundi.
Katika mchezo huo, pia matumizi ya VAR yalitumika kwa Mara ya kwanza Afrika katika ngazi ya taifa baada ya kuzinduliwa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Benin kwenye mchezo walimaliza leo ilicheza na  watu 10 baada ya Olivier Verdon kuonyeshwa kadi nyekundu na kubakia na idadi hiyo.

Author: Bruce Amani