Taifa Stars leo Machi 28 imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Libya kwenye mchezo wa kuwania kufuzu kucheza michuano ya Kombe la Mataifa Bingwa Afrika, (Afcon) uliochezwa Uwanja wa Mkapa Jijini Dsm.Bao pekee la ushindi kwa Stars lilipachikwa kimiani na Simon Msuva kunako dakika ya 45 kwa kichwa akiwa ndani ya 18.
Bao hilo lilidumu mpaka dakika 90 licha ya kipindi cha pili Libya kufanya mashambulizi makali matatu yaliokolewa na kipa Aishi Manula huku Stars wakiwa na kazi ya kulinda lango katika dakika za lala salama kwa kuwa wapinzani wao waliwaandama mwanzo mwisho.
Licha ya Stars kushinda imeongeza pointi zake tatu na kufikisha jumla ya pointi 7 ndani ya kundi J ila haina nafasi ya kufuzu Afcon kwa kuwa tayari Tunisia inayoongoza kundi ikiwa na pointi 16 na Equatorial Guinea yenye pointi 9 zimeshakata tiketi ya kwenda Cameroon wakati timu ya Libya imeshika mkia ikiwa ina alama tatu.
Author: Asifiwe Mbembela
Related Posts
-
Timu ya Madagascar yazawadiwa kwa kutinga AFCON
Serikali ya Madagascar imeitunuku timu ya taifa ya kandanda ya nchi hiyo kwa kufuzu kwa…
-
Cameroon yaanza vyema kampeni ya kutetea ubingwa Afcon
Mabingwa watetezi wa mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika AFCON Cameroon wameanza vizuri kwenye michuano…
-
Kenyatta aahidi kufanikisha maandalizi ya Stars baada ya kufuzu AFCON 2019
Rais Uhuru Kenyatta ameipongeza timu ya taifa ya soka ya Kenya Harambee Stars kwa kufuzu…
-
Madagascar yajikatia tikiti ya AFCON kwa mara ya kwanza
Madagascar imefuzu katika dimba la mataifa ya Kombe la Afrika – AFCON 2019 nchini Cameroon…
-
Taifa Stars hoi kwa Algeria
Taifa la Algeria limefanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora ya michuano ya Kimataifa Afrika Afcon…
-
Taifa Stars kamili gado kuwavaa Libya Afcon 2021
Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inashuka dimbani leo Jumapili Machi 28 kumenyana vikali…